Korea Kusini imesema imepata dalili kwamba Korea Kaskazini inajiandaa kufanya jaribio la tano la bomu la nyuklia, Rais Park Geun-hye amesema.
Hakufafanua zaidi kuhusu dalili hizo, lakini ameagiza jeshi la nchi yake kuwa tayari, shirika la habari la nchi hiyo limesema.
Kumekuwa na ripoti katika vyombo vya habari nchini Korea Kusini kwamba kumeongezeka shughuli katika kituo cha majaribio ya silaha za nyuklia cha Korea Kaskazini cha Punggye-ri, ambapo majaribio ya awali yalitekelezwa.
Iwapo Pyongyang itaendelea na kufanyia majaribio bomu la nyuklia, basi itakuwa ni kukaidi zaidi vikwazo vikali ilivyoongezewa na Umoja wa Mataifa mwezi jana.
"Tupo katika hali ya kutatanisha, hatujui iwapo Korea Kaskazini inaweza kufanya uchokozi kama njia ya kujitetea kutokana na kutengwa na jamii ya kimataifa na pia kuimarisha uungwaji mkono ndani ya nchi,” Bi Park aliambia maafisa wake wakuu wa jeshi, shirika la habari la Yonhap liliripoti.
No comments:
Post a Comment